Tunachoamini
Tunachoamini
Ona jinsi tunavyomwelewa Mungu, Yesu, Biblia, na mambo mengine muhimu ya imani yetu. Zikiwa zimejikita katika Maandiko, imani hizi zinaongoza maamuzi yetu kama huduma.
Biblia
Biblia ni Neno la Mungu kwa watu wote. Iliandikwa na waandishi wa kibinadamu chini ya uongozi wa ajabu wa Roho Mtakatifu. Kwa sababu iliongozwa na Mungu, Biblia ni kweli isiyo na mchanganyiko wowote wa makosa, nayo inafaa kabisa katika maisha yetu ya kila siku.
Yesu Kristo
Yesu Kristo ni mwanadamu kamili lakini, wakati huo huo, ni Mungu kamili. Yeye ndiye mpango pekee wa kuwarudisha watu waliomwacha Mungu kwenye uhusiano sahihi na Mungu. Aliishi maisha makamilifu, ili aweze kuwa mbadala wetu katika kutimiza matakwa ya Mungu ya ukamilifu. Aliishinda mauti katika ufufuo wake ili sisi tuweze kuwa na uzima.
Wokovu
Damu ya Yesu Kristo, iliyomwagika msalabani, ndiyo njia pekee ya wokovu kupitia msamaha wa dhambi. Wokovu hutokea watu wanapoweka imani yao katika kifo na ufufuo wa Kristo kama malipo yanayotosha kwa dhambi zao. Wokovu ni zawadi kutoka kwa Mungu, wala hauwezi kupatikana kwa juhudi zetu wenyewe.